Quantcast
Channel: MAMBO YA WALIMWENGU
Viewing all articles
Browse latest Browse all 2863

NJEMBA YAMNYWESHA MWENZAKE VIROBA TISA KISHA LAMHARIBU VIBAYA SEHEMU YA HAJA KUBWA.....

$
0
0
Singida
JESHI la Polisi mkoani Singida linamtafuta
 
kijana mmoja mkazi wa Kibaoni katika
 
manispaa hiyo kwa tuhuma za kumlawiti
 
mwenzake na kumharibu vibaya sehemu za haja
 
kubwa baada ya kumnunulia pombe kali aina
 
ya viroba jogoo tisa.
 
Kamanda wa polisi mkoani hapa, Geofrey
 
Kamwela, alisema kuwa tukio hilo lilitokea juzi
 
saa 3:00 usiku eneo la soko la Kibaoni, kata ya
 
Kindai, na kumtaja mtuhumiwa huyo kwa jina
 
moja la Athuman.
 
Alisema kuwa baada ya kila mmoja kumaliza
 
kunywa viroba vyake, kijana aliyelawitiwa (jina
 
tunalihifadhi) alimweleza mtuhumiwa kuwa
 
amelewa kupindukia na hivyo kila mmoja
 
arejee nyumbani kwao.
 
“Walipofika eneo la soko la Kindai, muathirika
 
alimwambia mtuhumiwa amwache hapo ili
 
apumzike kwa vile pombe ilikuwa imemzidi
 
sana lakini ghafla alianguka chini na kisha na
 
kupoteza fahamu,” alisema.
 
Baada ya muathirika kupoteza fahamu,
 
mtuhumiwa alitumia fursa hiyo na kuanza
 
kumwingilia kimwili kinyume cha maumbile.
 
Alisema kuwa wasamaria wema walimshuhudia
 
mtuhumiwa akiendelea kufanya unyama huo
 
dhidi ya rafiki yake lakini walipojaribu
 
kumkamata, aliwaponyoka na kukimbilia
 
kusikojulikana.
“Raia wema hao walimbeba muathirika na
 
kumpeleka nyumbani kwake na baadaye aliweza
 
kupata fahamu ndipo alianza kusikia maumivu
 
makali sehemu yake ya haja kubwa,” alisema.
 
Alisema muathirika alipelekwa hospitali ya
 
mkoa wa Singida ambako alibainika kuharibiwa
 
vibaya sehemu zake za haja kubwa.

Viewing all articles
Browse latest Browse all 2863

Trending Articles