![]() |
Hali ya Nisha ilivyo kwa sasa. Hapa akilazimishwa kula chakula. |
Maskini! Staa wa sinema za Kibongo, Salma Jabu ‘Nisha’ anateseka baada ya kupata gonjwa la ajabu linalomsababishia maumivu makali.
Akizungumza rafiki yake ambaye pia ni msanii mwenzake, Happy John ‘Nyatawe’ alisema Nisha alianza kulalamika kwamba anasikia vitu vikimtembea mwilini na maumivu makali ya kichwa kinachomuuma mfululizo.
“Alianza kulalamika kuumwa kama mchezo lakini siku zinavyozidi kusonga ndivyo hali yake inavyozidi kuwa mbaya, hata hatuelewi ni nini,” alisema Nyatawe.
Paparazi wetu alifanikiwa kuzungumza na Nisha akiwa nyumbani kwake huku akilishwa chakula kama mtoto ambapo alisema anasikia maumivu makali ya kichwa na tayari ameshaenda hospitali akapewa dawa lakini ugonjwa unaomsumbua haukujulikana.
Wakati paparazi wetu akiendelea na mazungumzo hayo alimshuhudia Nisha akiweweseka kama mtu aliyechanganyikiwa.
KUNA MKONO WA MTU
-gpl