Quantcast
Channel: MAMBO YA WALIMWENGU
Viewing all articles
Browse latest Browse all 2863

MASKINI NISHA..APATA GONJWA LA AJABU FULL UTATA..SOMA ZAIDI HAPA...!

$
0
0
Hali ya Nisha ilivyo kwa sasa. Hapa akilazimishwa kula chakula.
Maskini! Staa wa sinema za Kibongo, Salma Jabu ‘Nisha’ anateseka baada ya kupata gonjwa la ajabu linalomsababishia maumivu makali.
“Alianza kulalamika kuumwa kama mchezo lakini siku zinavyozidi kusonga ndivyo hali yake inavyozidi kuwa mbaya, hata hatuelewi ni nini,” alisema Nyatawe.
 Paparazi wetu alifanikiwa kuzungumza na Nisha akiwa nyumbani kwake huku akilishwa chakula kama mtoto ambapo alisema anasikia maumivu makali ya kichwa na tayari ameshaenda hospitali akapewa dawa lakini ugonjwa unaomsumbua haukujulikana.

 
Nisha akilishwa chakula.
 “Kichwa kinaniuma sana na vitu vinanitembea mwilini sijielewi kabisa, muda mwingine ninakandwa na maji ya baridi kutokana na maumivu makali, nimeenda hospitali nimepima kila kitu lakini ugonjwa hauonekani,” alisema Nisha akitokwa machozi kutokana na maumivu aliyokuwa akiyasikia.
 Wakati paparazi wetu akiendelea na mazungumzo hayo alimshuhudia Nisha akiweweseka kama mtu aliyechanganyikiwa.
 KUNA MKONO WA MTU
Baadhi ya wasanii ambao hawakutaka kutajwa walisema kutokana na hali aliyonayo Nisha inawezekana kuna mkono wa mtu kwani wasanii wamezidi kwa kulogana hivyo anatakiwa kuombewa kwa Mola kwani hali ya afya yake si shwari.
-gpl

Viewing all articles
Browse latest Browse all 2863

Trending Articles