Waraka mwingine ulioandikwa katika lugha ya Kiswahili umechapishwa hapo chini … Waraka huo unataja majina ya Watanzania wawili kuwa wafanyabiashara wa dawa za kulevya.
Waraka huo wenye saini ya aliyejiita Jumaa, akiwa jela Hon Kong, ni wa kurasa mbili zilizojaa maneno ya kujuta kwa kufanya kazi hiyo haramu. Ni waraka ambao unaeleza mbinu mpya inayotumiwa na wafanyabiashara hao haramu kwa kuwatoa kafara Watanzania wanaokubali kuwa punda wa kubeba dawa hizo.
Mwishowe unatoa onyo kwa kila Mtanzania anayejiingiza katika biashara hiyo na kutoa wito wa kusambaza taarifa hii ili kuwaonya watu wengine wasithubutu kujiingiza katika biashara hiyo haramu.
credirt: domo langu website